Tuesday, August 21, 2012

KILWA KIVINJE NA IDD EL FITR vs SENSA - 20/8/2012

Isihaka Mchinjita posted in INTER ISLAMIC SCHOOLS TZ -20/8/2012


  Mkuu wa wilaya kilwa, Mkoa wa Lindi,  anusurika kupigwa Kilwa Kivinje

Mkuu wa wilaya ya Kilwa ametolewa msikiti wa  Al az har, mjini Kivinje chini ya ulinzi wa
  viongozi wa msikiti baada ya kuwataka waislamu kushiriki sensa.

Awali mkuu huyo wa wilaya alichangia Tsh.1,000,000 kwa ukarabati wa msikiti  ambapo baadae alibeza
  msambazaji wa vipeperushi vinavyowataka waislamu kutoshiriki sensa mpaka
  kipengele cha dini kiwekwe.

Baada ya kauli yake hiyo waislamu walinyoosha mikono msikiti mzima wakitaka kumhoji.kufuatia hali hiyo viongozi  walisimama kutaka kuzuwia hali hiyo na hapo zogo likatokea na mashekh  kuamua kumtoa mkuu huyo huku wakilaumiwa na waumini na hivyo kuondoka   msikitini hapo bila hata kuomba duwa.

Hali hii imemfanya mkuu wa wilaya kutozungumzia sensa baadae alipokuwa kwenye Baraza la Eid  el Fitr, ambapo pia alialikwa kama mgeni rasmi.




HIZI  NI  SALAM  TOSHA KWAMBA WAISLAM WA KILA KIVINJE  WAMESIMAMA KIDETE KUTETEA DINI YAO NA KUONDOA MUNKAR KWA MIKONO YAO. 

No comments:

Post a Comment