Sunday, March 29, 2009

TOFAUTI KATIKA VIUMBE WA MWENYEZIMUNGU

Imechangiwa na Dada Saada al-Ghafry.

Kuna waganga wa kitabu wa kweli na matapeli, lakini kwa Tanzania wengi wao ni matapeli. Mganga akishakwambia "umefanyiwa hivi na xyz ", mara nyingi huyo xyz akiwa ni mpenzi wa aina moja ama nyingine kama ni kwenye familia au urafiki, ujue huyo ni tapeli. Kimbia haraka sana. Yapo matibabu ya Kitabu, lakini ni wachache sana wenye ujuzi huo, na tiba hiyo haistahili kupokea malipo.
Majini yapo, na ni kweli yapo mazuri na mabaya, kama walivyo wanadamu wazuri na wabaya. Vitendo vyema (vinavyotekeza amri za Mwenyeezi Mungu) vinamfanya jini na binaadamu wajulikane kuwa ni wazuri na wale wenye vitendo vibaya (vinavyoasi amri za Mwenyeezi Mungu) vinamfanya jini na binaadamu wajulikane kuwa wabaya. Sote ni viumbe wa Mwenyeezi Mungu kama walivyo wanyama na Malaika pia kuwa ni viumbe wa Mwenyeezi Mungu. Sote tumeumbwa ili tumuabudu Mwenyeezi Mungu. Binadamu na wanyama tunaonekana, Malaika na majini hawaonekani nasi ila kwa wenye elimu ya majini km Nabii Daud aliweza kuwafuga na kuwatuma majini. Wapo pia hivi sasa wenye elimu ya kufuga na kuwatumikisha majini, lakini Mwenyeezi Mungu amekataza shughuli hiyo. Nabii Daud alipewa ruhusa maalum, wengine hawaa ruhusa hiyo.
Kwa Kiarabu anaitwa jinn, na kwa Kiinglish anaitwa genie.

HARAMU YA KUTABIRI KATIKA UISLAM

Imechangiwa na Bi Saada al-Ghafry.

Utabiri kwenye Uislam ni haram. Hakuna iitiradhi katika hilo. "Ilm alghaaib" ni ya Mwenyeezi Mungu peke yake. Haina mshirika.

Kuwa na elimu kuliko wengine ni neema kutoka kwa Mwenyeezi Mungu. Kuitumia vibaya (kwa kwenda kinyume ya maamrisho yake) ni dhambi. Ndiyo utakuta daktari anakwambia mgonjwa ana saa/siku/miezi/miaka kadhaa ya kuishi. Mwenyeezi Mungu anamuumbua. Anakufa daktari na mgonjwa anapona. Cha kusema ni kuwa sisi tunafanya kilicho kwenye uwezo wetu, yaliyobaki tunamwachia mwenye milki ya uhai na mauti.

Zoezi la unajimu, kwa watendaji na wafuasi, ni ushirikina kwenye Uislamu. Yahya Kufanya utabiri hakuhalalishi alichoharamisha Mwenyeezi Mungu, kama vile mapadre kulawiti watoto ni haram. Liwati haihalalishwi kwa vile mapdre wanafanya hivyo.

Ni mengi yaliyoharamishwa lakini yanafanywa. Ni lazima turudi kwenye vitabu na sio kuwatazama au kuwasikiliza wanaodai kuwa ni wafuasi wa vitabu.

Friday, March 27, 2009

UONGEZAJI WA UPEKUZI SAFARI ZA ANGA

A response on passenger Screening Rules being expanded:
Imechangiwa na Bi Saada al-Ghafry.


Hakuna binaadamu anaeweza kukuhakikishia usalama wako
bali Allah peke yake ndiyo mwenye uwezo huo. Watu wengi
zaidi wanakufa barabarani kuliko ajali zote za usafiri hewani,
sikwambii asilimia ndogo kati ya ajali hizo za hewani kuwa
ni waathirika wa kutekwa nyara. Lakini hatuachi kuendesha gari
au kuwa wasafiri kwenye magari. Uthibitishiwe usalama ama
la, malik al mawt akikusimamia huna ujanja...
Mimi nakubali kabisa kuwa ukaguzi ni muhimu. Nimesafiri miaka
nenda rudi kabla ya 9/11 ukaguzi ulikuwepo. Nisichokubali
ni ubaguzi kwenye ukaguzi. Ubaguzi wa kuchagua jina na
rangi.
Niliwahi kusafiri kwenda Tanzania, dakika chache baada
ya kupaa Jeddah, nikasikia mpasuko na ndege ikayumba.
Waliokuwa wamelala wakashtuka. Kila mmoja akawa na
wasiwasi kumetokea nini, mimi niko kwenye dua tu huku
nimemkumbatia mwanangu. Hatimaye tukaelezwa kuwa
injini moja ina matatizo (hatukuelezwa ni matatizo gani).
Hatukuweza kuendelea na safari kuelekea Dar maana
hakuna ufundi, hatukuweza kurudi Jeddah kwa sababu
ya sheria za uhamiaji, ikabidi twende Zurich.
Chuma si lazima kitolewe na abiria mwingine tu. Ndege
nzima ni chuma kinachoweza "kuwaangusha" wakati
wowote.
Tawwakul, Mzee wangu, Tawwakul ndiyo usalama wako.
Likikufika, zako zimefika. Hakuna dawa. Ni sababu tu.

MABADILIKO YA WAKUU WA WILAYA TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya chini kwa kuwateua wapya 15, kuwastaafisha wengine saba na kuwabadilisha vituo vya kazi 54.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) imeonyesha pia kuwa Wakuu wa Wilaya wawili watapangiwa kazi nyingine na wengine wawili wameteuliwa hivi karibuni kuongoza Jumuiya za Chama Tawala.

Mabadiliko haya yanatarajiwa kuongeza chachu katika usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za maendeleo ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake, kwa mujibu wa taarifa hiyo.

Wakuu wapya wa Wilaya walioteuliwa ni Bi. Mercy Silla (Arumeru, Arusha), Bw. Norman Sigalla (Hai, Kilimanjaro), Col. Issa E. Njiku (Misenyi, Kagera), Bi. Angelina Mabula (Karagwe, Kagera), Dkt. Rehema Nchimbi (Newala - Mtwara), Francis Isaac (Mbulu, Manyara), Lt. Col. Benedict K. Kitenga (Rorya, Mara) na Lt. Col. Cosmas Kayombo (Mbarali, Mbeya).

Wengine ni Bw. Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba, Mwanza); Bi. Queen Mwanshinga Mlozi (Ukerewe, Mwanza); Bi. Fatuma Mwassa (Mvomero, Morogoro); Bi. Fatma Ally (Nanyumbu, Mtwara); Bw. Juma Solomon Madaha (Tunduru, Ruvuma); Bw. Anatory Choya (Kishapu, Shinyanga) na Bw. Erasto Sima (Korogwe, Tanga).

Wakuu wa Wilaya waliostaafishwa na vituo vyao kwenye mabano ni Bw. Elias Maarugu (Misenyi, Kagera); Bw. Deusdedit Mtambalike (Muleba, Kagera); Bw. David Holela (Babati, Manyara); Bi. Hawa Ngulume (Mbarali, Mbeya); Bw. Mashimba H. Mashimba (Kyela, Mbeya); Col. Peter Madaha (Nyamagana, Mwanza) na Bw. Gilbert Dololo (Kibaha , Pwani).

Wakuu wa Wilaya ambao wamepangiwa kupewa kazi nyingine ni Bw. Patrick Tsere aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala (Dar es Salaam) na Bi. Doreen Kisamo aliyekuwa Uyui (Tabora).

Bw. Martin Shigela aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi (Lindi) aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM wakati Bi. Husna Mwilima aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai (Kilimanjaro) aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UWT.

Wakuu wa Wilaya waliobadilishwa vituo vya kazi ni hawa wafuatao:

Na.

JINA

KITUO CHA SASA

KITUO KIPYA

(Wilaya)

MKOA

Wilaya

  1. 1

Elias W. Lali

Arusha

Arumeru

Ngorongoro

  1. 2

Evans Balama

Arusha

Arusha

Ilala

  1. 3

Jowiko W. Kasunga

Arusha

Ngorongoro

Monduli

Col. Fabian I. Massawe

D’salaam

Kinondoni

Muleba

Abdallah A. Kihato

D’salaam

Temeke

Kyela

Bi. Zainab Kwikwega

Dodoma

Bahi

Kasulu

Dk. Ian J. Langiboli

Dodoma

Chamwino

Babati

Capt. Seif A. Mpembenwe

Dodoma

Kondoa

Handeni

Bi. Halima Dendego

Dodoma

Mpwapwa

Kilosa

Lephy B. Gembe

Iringa

Makete

Chamwino

Elaston J. Mbwilo

Iringa

Iringa

Mtwara

Bibi Darry I. Rwegasira

Iringa

Njombe

Mpwapwa

Said M. Mkumbo

Kagera

Chato

Temeke

Frank A. Uhahula

Kagera

Karagwe

Tarime

Lt. Col. John Mzurikwao

Kigoma

Kibondo

Mpanda

Saidi Bwanamdogo

Kigoma

Kasulu

Kondoa

Raymond H. Mushi

Kilimanjaro

Rombo

Arusha

Jordan Rugimbana

Kilimanjaro

Mwanga

Kinondoni

Rashid M. Ndaile

Lindi

Nachingwea

Chunya

Anna Magowa

Lindi

Liwale

Hanang

Elias Goroi

Manyara

Mbulu

Nachingwea

Capt. Geoffrey Ngatuni

Manyara

Hanang

Musoma

Saveli Maketta

Mara

Musoma

Namtumbo

Stanley Kolimba

Mara

Tarime

Uyui

Bibi Miriam L. Lugaila

Mbeya

Rungwe

Misungwi

Halima Kihemba

Mbeya

Mbozi

Kibaha

Bibi Fatuma L. Kimario

Mbeya

Chunya

Igunga

Athuman H. Mdoe

Morogoro

Kilosa

Mwanga

Hawa Ng’humbi

Morogoro

Mvomero

Makete

Gishuli M. Charles

Mtwara

Mtwara

Njombe

Jackson W. Msome

Mtwara

Newala

Rungwe

Capt. Assary Geofrey Msangi

Mtwara

Nanyumbu

Iringa

Samwel Kamote

Mwanza

Ilemela

Bukoba

Danhi Makanga

Mwanza

Kwimba

Kibondo

Magalula S. Magalula

Mwanza

Misungwi

Lindi

Paul Chiwile

Mwanza

Ukerewe

Liwale

Mathew K. Nasei

Mwanza

Magu

Muheza

Lt. Col. Serenge M. Mrengo

Pwani

Bagamoyo

Ilemela

Ali N. Rufunga

Pwani

Rufiji

Manyoni

Meja Bahati Matala

Rukwa

Sumbawanga

Kahama

Thobias Mazanzala

Rukwa

Mpanda

Sumbawanga

Gabriel Kimolo

Ruvuma

Namtumbo

Mbozi

Peter Toima Kiroya

Ruvuma

Tunduru

Rombo

Amina Masenza

Ruvuma

Mbinga

Shinyanga

Khadija R.R. Nyembo

Shinyanga

Kishapu

Chato

Col. (Mst) Edmund Mjengwa

Shinyanga

Shinyanga

Mbinga

Magesa Mulongo

Shinyanga

Bukombe

Bagamoyo

Bibi Florence A. Horombe

Singida

Singida

Bukombe

Pascal Mabiti

Singida

Manyoni

Singida

Cleophas Rugarabamu

Tabora

Igunga

Nyamagana

Kassim Majaliwa Majaliwa

Tabora

Urambo

Rufiji

Lt. Winfrid F. Ligubi

Tanga

Handeni

Urambo

Elizabeth Mkwasa

Tanga

Korogwe

Bahi

Zainab Kondo

Tanga

Muheza

Magu