Friday, November 30, 2012

UTEKELEZAJI WA "EVANGELIZING MUSLIMS" NCHINI TANZANIA

On Nov 27, 2012 4:22 PM, "Mohamed Issa" <hemedshk@gmail.com> wrote:
 

Assalaam alaykum.
 
Allah anatuambia katika Qur'an "Na hawatoacha kukupigeni vita mpaka wakuritadisheni kutoka kwenye dini yenu wakiweza.." (Al Baqarah 2:217)

Siku ya Jumamosi terehe 24 Novemba, 2012 itaingia katika maisha yangu ya da’wah kama siku niliyoona kivitendo jinsi ambavyo mipango iliyowekwa na wakristo kupitia mafunzo maalum yaitwayo “Evangelizing Muslims” inavyoweza kuwatoa waislamu kutoka katika Uislamu wao.

Nilialikwa kuhudhuria sherehe za ufungaji wa shule ya Kiislamu Iqra English Medium School inayoendeshwa na Pahi Islamic Center, taasisi iliyosajiliwa yenye Makao yake Makuu kijiji cha Pahi, Tarafa ya Pahi, Wilaya ya Kondoa yenye waislamu takriban 95%. Kondoa kuna vijiji huwezi kukuta mkristo hat ammoja lakini hivi sasa kuna kasi kubwa ya kuwaritadisha waislamu.

Ninaambiwa kwamba mnamo miaka ya 1998-2000, walifika wazungu watatu wakiwemo Wamarekani wawili (wanawake) na Mjerumani mmoja. Walifika wakidai kutaka kujifunza lugha na mila za kabila la warangi. Wakapokelewa na ndugu mmoja aitwaye Halifa Nchasi (ambaye sasa ndiye Katibu wa Pahi Islamic Center) na ndugu huyu akawafundisha hawa wazungu kirangi kwa muda wa wiki tatu na wakakimudu vizuri (walikuwa wataalam wa lugha).

Wale wanawake walifikia kuishi maisha ya mwanamke wa kawaida wa kirangi wakishiriki shughuli zote zifanywazo na mwanamke wa kabila hili kuanzia kuteka maji, kukata kuni hadi kubeba mtoto mgongoni na wakapewa majina ya kirangi-mmoja akiitwa Mwasu na mwingine Sware. Baada ya muda, jamaa hawa wakaja kuanzisha mradi uitwao “COMPASSION” ambao ulilenga kuwasaidi awaislamau masikini husuusan katika huduma ya afya.

Wakaanza kumimina misaada kutoka huko ughaibuni wakianzia na kuweka magari matatu katika vijiji vitatu- moja pahi kwenyewe, jingine Kinyasi na jingine Salare kwa ajili ya kubeba wagonjwa kwa kila mwenye mgonjwa kuchangia fedha ya mafuta tu Sh 10,000 kuepelekewa mgonjwa wake hospitalai ya Wilaya Kondoa mjini kwani tarafa nzima ya pahi haina hospitali. Wapashajai ahabari wangu wananiambia kwamba mara baada ya waazungu hawa kuja Pahi, malaria ya ajabu ilizuka. Wanaamini kwamba wazungu hawa walipandikiza mbu mwenye vimelea vya malaria.

Baadaye wazungu hawa wakaomba kupataiwa ekari 7 ili wajenge zahanati hapo Pahi. Uongozi wa serikali ya kijiji ukaitish amkutano wa hadhara na kuwataka ushauri wanakijiji ambao 99% ni waislamu. Kutokana na “wema” waliofanyiwa, wanakijiji wote wakaunga mkono wakristo hao kupatiwa ardhi waliyoomba. Wakrsito wakajenga zahanai yao na ikawa pia andiyo kituo cha kuwakusanya wale waislamu masikini kwa ajili ya mafunzo maalum kila jumamosi ambapo wakitoka huko hupatiwa mche wa sabuni, madaftari n.k.

Kilichofuatia ni jamaa kuomba atrdhi nyingine ekari 7 kwa ajili ya kujenga shule ya wasichana. Hivi sasa wanaendesha shule ya wasichana (boarding na day) yenye kuchukua wasichana 600 na kila mwaka ninaambiwa takriban wasichana waislamu 5-10 huritadi. Hata wale amabo hawajaritadi, huonesha wazi kuwa wameugura Uislamu kwa sababu wanapopita njiani wakawaona waislamu husuusan akina mama waliojisitiri husikika wakisema “Mashetani hao”.

Kubwa zaidi hiyo COMPASSION imeanzisha mtindo wa “Family Friends” ambapo familia moja masikini ya kiislamu huunganishwa na familia ya kikristo huko Ulaya ana Marekani na hiyo familia ya nje huisaidia familia ya ndani kwa hali na mali. Hili nalo limezidisha hatarii ya waislamu kuritadishwa na tayari familia kadhaa zimesharitadi familia nzima.

Kibaya zaidi, waislamu hapo Pahi wamegawanyika wakipigana vita. Answar Sunnah wamegawika makaundi mawili yenye kupingana na hawa wanaosema wao ni Bakwata pia ni faraqa tu. Hali ya Paahi na vijiji vingi vya Kondoa ni mbaya. Kingine cha kuzingatia Kondoa sasa ni Jimbo la Kanisa Katoliki lenye Askofu wake kamili.

Nimefanya fikra na waislamau pale na ndugu zetu wa Morogoro kwa ajili ya kuunusuru Uislamau pale. Yapo yaliyoazimiwa ambayo siwezi kuyaweka bayana humu bali niwatangazie tu biashara kwamba wale wenye Ilmu wanaaweza kuitembelea Pahi na kufanya da’wah. Pia wale ambao hatuna Ilmu, ikifikia wakati nguvu zikahitajika nasi tuwe tayari. Pahi imetengewa Tshs 10,000,000 kila mwaka kwa ajili ya kuritadisha waislamu.

Inasemekana wazungu hawa walisoma kwenye Mtandao kwamba Paahi ni Markaz Kuu ya Fisabiylillahi Marakaz barani Afrika. Ni kweli pahi kulifunguliwa Markazi Kuu ya Fiysabiilillahai Afrika mwaka 1981. Hadi sasa kuna ekari 110 zimekaa tu pasina kutumika mbali na msikiti uliowekwa jiwe la msingi na aliyekuwa Makamu wa Rais wakati huo Mzee Aboud Jumbe. Huu naoa ni udhaifu mkubwa wa taasisi hiyo. Pia kuna taasisi nyingine iitwayo IDA inazo ekari 16 nazo zimelala pasina kufanayika chochote hapo kwa miaka sasa. Watu wako tayari kinachokosekana ni uongozi na maelekezo.

Huu ni mfano tu kwani najua hali ndiyo hii sehemu kubwa ya nchi. Ukizingatia kwamba wakristo wana hiyo MoU yao na Serikali kutengewa mabilioni kwa ajili ya elimu, afya na huduma nyingine za jamii, bila shaka kasi ya kuwaritadisha waislamu itaongezeka.

--
Sheikh Muhammad Issa
(Private Mail)
Youtube Channel" Mohamed Issa

1 comment:

  1. I had very small penis, not nice enough to satisfy a woman had many relationship called off it became an embarrassment which i couldn't afford to bear no more because i had so e relationship called off because of my situation, then I started searching for solutions cause I knew if I didn't find a solution it would eventually end my sex life then I came across saw some few comments about Dr Ekpen then  decided to email him on so I decided to give his herbal product a try then we discussed, he then gave me some comforting words and also gave his herbal cream for Penis enlargement cream and pills, Within 7 days of usage of it, i began to feel the enlargement of my penis, and now after 2 weeks of using his products my penis is about 10inches I couldn't wish for anything in life other than to be free from this predicament and Dr Ekpen medication gave me the Result I badly needed longer email him to get your issue solved just like he solved mine contact (Email: doctorekpen222@gmail.com) or  whatsapp  +2348102454875   also have cure to all kind of diseases

    ReplyDelete